Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Sunday, June 27, 2010

BANDA LA KAMPUNI YA MAKAI MORINGA (MLONGE) ENTERPRISES KUPAMBWA NA WAREMBO WA MISS UTALII SABASABA MWAKA HUU


Eileen Kasubi Katikati akiwa na warembo wanaowania taji la Miss Utalii Tanzania Kampuni ya Makai Moringa (Mlonge) Enterprises ni moja ya wadhamini wa mashindano hayo


TAARIFA KWA VYOMBO KWA HABARI

Ndugu waandishi wa habari Jina langu ni Eileen Kasubi , Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Makai Moringa (Mlonge) Enterprises ambayo inajushughulisha na ulimaji na uzalishaji wa bidhaa mbalimbali zitokanazo na mti wa mlonge kwa zaidi ya miaka 8 sasa.

Tulishirikiana na kampuni ya kimataifa ya Optima of Africa, tulihamasisha kilimo cha mti wa zao hilo na kununua mazao yake kwa wakulima .

Mlonge ni mti wa maajabu kwani ni lishe,kinga na tiba kwa zaidi ya magonjwa 300 ya binadamu. Bidhaa zote za mlonge zinazotengenezwa na Makai Enterprises ni bora na zimethibitishwa na Mkemia Mkuu wa Serikali na Mamlaka zote za kitaifa na mataifa.

Bidhaa hizo zinatokana na majani, mbegu,mizizi na mti wenyewe wa Mlonge kwa kutengeneza virutubisho asili,vipodozi, na madawa ya mwili wa binadamu.

Awali tulikuwa na bidhaa kuu 8 ambazo ni
1)Unga wa majani ya Mlonge ambao ni lishe, tiba na kinga zaidi ya magonjwa 300 inalinda afya ya binadamu pamoja na kurutubisha mifumo mbalimbali ya mwili.
2)Mbegu za Mlonge hutibu Malaria, Saratani ya tumbo,hupungusa sonona stress, huleta hamu ya kunywa maji,huongeza kinga ya mwili CD4s
3) Mafuta ya Mlonge ya kula huua sumu ndani ya chakula, huua aina nyingi za bacteria kwenye chakula na huondoa cholesterol
4)Mafuta ya kupaka mwilini (Moringa skin care oil) huondoa fangazi kwenye ngozi, chunusi, harara makovu pamoja na mba mwilini
5)Mafuta ya kuchua (Moringa Massage Oil) Huondoa maumivu ya mgongo, kiuno, miguu, hutibu baridi ya-bisi na hupasha misuli joto.
6)Sabuni ya kuogea (Moringa Toilet soap) Hutibu magonjwa mbali mbali ya ya ngozi,fangazi, chunusi ,mba na hulinda ngozi yako
7)Mafuta ya nywele (Moringa Hair food)hung’arisha na kuimarisha nywele huondoa mba na mapunye kichwani na kurefusha nywele.
8)Moringa Sports Ointment (Mafuta ya wana michezo) Huondoa maumivu ya misuli inayokakamaa na hushtua neva na misuli iliyolala kutokana na maumivu au kutokana na kiharusi.

Nafurahi kuwajulisha kuwa leo hii tunazindua bidhaa zetu mpya
ambazo ni:-
1) Moripower - Inaongeza nguvu za kiume
2)Moribites - Inatibu Kisukari
3)Morident - Tiba ya Meno)
4)Moringa Shampoo - Inaondoa mba na miwasho yote kichwani , Inaondoa uchafu kichwani kwa nywele za aina yote
5)Moringa Face & Body Scrub -Huondoa madoa, chunusi usoni, mgonngoni, na sehemu zote za mwili
6)Moringa Body Shower - Sabuni ya Maji ya Kuogea
7)Moringa Hand wash Sabuni Asili ya kunawia mikono
8)Moringa Detergent and Disnfectant - Dawa za kusafishia sakafu,vyoo na masink
9)Sabuni Mwaniki (Ladies Soap) - Sabuni maalum na nyeti kwa kina mama humaliza fangazi katikati ya mapaja na kwapani .

Kutokana na mabadiliko ya kisayansi na teknologia, matumizi ya bidhaa zenye kemikali yamekuwa yakiongezeka kila siku, huku madhara yake yakiadhiri maisha ya kila siku ya binadamu, kuanzia katika vipodozi, tiba na usafishaji. Ndio maana leo hii tunawashuhudia watu wakiishi maisha mafupi kuliko awali, watu kuonekana wazee kuliko umri wao, magonjwa ya ngozi huongezeka na hata wanaume wengi kupoteza ulijari na nguvu asili za kiume, wakati mwingine baadhi ya magonjwa hujenga sugu ya kutotibika.

Tumeamua kuwatumia na tunawashukuru sana warembo wa Miss Utalii Tanzania, kuzindua Bidhaa hizi za mlonge, kutokana na ukweli kuwa wamekuwa msitari wa mbele kuhamasisha utamaduni na utunzaji wa misitu ya nchi, ambako mlonge pia unatoka. Tutawatumia pia warembo hawa katika maonyesho ya kitaifa 7/7 mwaka huu, ambako bidhaa hizi zitapatikana katika banda letu liliopo katika mabanda mapya ya 7/7 , Banda la Maliasili na Utalii na Banda la SIDO .

Mwisho nitoe wito kwa watu wote kutumia bidhaa asili za Mlonge uliotengenezwa na Makai kwa maisha marefu zaidi. Tayari bidhaa hizi zimepata soko katika nchi mbai mbali duniani zikiwemo Ujerumani, Marekani, Denmark, Japan, Africa Kusini, Malawi na nchi nyinginezo.

Ofisi zetu zipo:-
Pamba House G0orofa ya Pili Chumba No. 205
Simu No. + 255 2135531/ 0713 607408/0787 607408
0767 838188
Email: makaimlonge@yahoo.com

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...