Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Monday, September 27, 2010

MASHINDANO YA ‘Rock City Marathon 2010’ YAFANA


Na Mwandishi Wetu
MWANARIADHA Daudi Joseph na Polnes Chacha wameibuka vinara katika mashindano ya
riadha kilometa 21 yanayojulikana kama ‘Rock City Marathon 2010’ yaliyofanyika
Jijini Mwanza Jumapili.
Joseph alishinda mbio hizo kwa upande wa wanaume baada ya kuchukua saa 1:03:40
huku mwanadada Chacha akishinda kwa upande wa wanawake baada ya kutumia saa
1:13:10.Zaidi ya wanariadha 200 walijitokeza kushiriki mashindano hayo.

Wanaume walionekana kuwa na mchuano mkali kutokana na kutopishana sana kumaliza
mbio hizo ambapo Eliya Sidame alishika nafasi ya pili baada ya kupishana na
mshindi kwa sekunde 10 ambapo yeye alitumia saa 1:03:50.
Nafasi ya tatu kwa wanaume ilikwenda kwa Ezekiel Japhet aliyetumia saa 1:04:05
ikiwa ni tofauti ya sekunde 15 na aliyeshika nafasi ya pili na sekunde 25 na
Joseph aliyekuwa kinara wakati kwa wanawake Jacquline Juma alishika nafasi ya
pili kwa kutumia saa 1:18:09 na nafasi ya tatu ilikwenda kwa Rebeka Chacha
aliyetumia saa 1:19:05.
Katika mbio za kilometa 5, Mzungu Ndorobo alishinda na kufuatiwa na Victor
Daniel aliyekuwa wa pili na Dotto Ikangaa akishika nafasi ya tatu wakati katika
mbio za kilometa 3 ambazo zilikuwa maalumu kwa wazee, Jonas Mwangole alishika
nafasi ya kwanza akifuatiwa na Ramadhani Kinye aliyeshika nafasi ya pili.
Kwa upande wa wanawake kilometa 5 mshindi alikuwa Fazina Rashid akifuatiwa na
Saida Romanus aliyeshika nafasi ya pili huku nafasi ya tatu ikienda kwa Godriver

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...