Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Monday, November 15, 2010

SIR ALEX FERGUSON ASEMA ROONE ATAREJEA KIKOSINI



KOCHA Sir Alex Ferguson amesema kuwa
Wayne Rooney atarejea katika timu ya Manchester United leo baada ya timu yake kutoka sare ya bao 2-2 dhidi ya Aston Villa.

United iliweza kuendeleza rekodi yake ya kutofungwa katika mechi za msimu huu baada ya kucheza mechi 26, mwishoni mwa wiki walilazimika kutoka na nyuma na kusawazisha mabao mawili yaliyofungwa na Federico Macheda na Nemanja Vidic hivyo kupata pointi katika uwanja wa Villa Park Jumamosi.

Ferguson aliwasifu wachezaji wake kwa kucheza kwa kujituma baada ya kufungwa na kusawazisha, sasa atamwongeza Rooney baada ya kurejea katika uwanja wa mazoezi wa United, Carrington.

Rooney alisafiri kwenye marekana na kukaa kwa wiki moja na kufanya mazoezi ya viungo baada ya kuumia enka, anatarajiwa kucheza Jumamosi katika mchezo kati ya England dhidi ya Wigan .

Ferguson alisema: "Wayne alikuwa na wiki nzuri. Alifanya mazoezi ya nguvu. Alikuwa na vipinzi viwili vya maoezi kwa siku na kufanikiwa kile alichokuwa akitakae."

United iko katika nafasi ya pili hasi hana ilikuwa ikizidiwa pointi tatu dhidi ya Chelsea ambayo ilikuwa na me dhidi ya Sunderland.

Ferguson amesema kuwa bado wako katika mbilo za kuwania ubingwa unaoshikiliwa na vijana wa Carlo Ancelotti.

Ashley Young alifunga kwa penalti goli la kwanza na kisha Marc Albrighton alifunga bao la pili na kuipatia matumaini Villa kupata ushindi wa kwanza dhidi ya Fergusontangu mwaka 1995.

Lakini United ilipata goli kupingi kwa mcheaji aliyetokea benchi Macheda na kisha Vidic alifunga goli la kusawazisha na kufanya timu yake kupata pointi moja.

Kocha wa Villa, Gerard Houllier alisema timu yake ilishindwa kutoka na ushindi kutokana na kwua na wachezaji wasiokuwa na uzoefu na kuongeza kuwa kwa uchezaji wao watakuja kuwa wazuri baadaye baada ya kuichukua timu Septemba.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...