Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Tuesday, April 5, 2011

PICHA ZA MKUTANO WA TATU WA BUNGE ULIOANZA MJINI DODOMA LEO











Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Anne Makinda akiingia ndani ya ukumbi wa Bunge kuongoza kikao cha kwanza cha mkutano wa tatu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania leo mjini Dodoma.



Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Anne Makinda akitoa ufafanuzi kwa wabunge kuhusu kanuni za uendeshaji wa shughuli za bunge leo mjini Dodoma.



Waziri wa Sheria na Katiba Celina Kombani akitoa ufafanuzi kwa wabunge kuhusu namna ya kuingia katika zoezi la upatikanaji wa katiba mpya na namna wananchi watakavyoshiriki kutoa maoni yao katika mchakato wa upatikanaji wa katiba hiyo bungeni mjini Dodoma.



Waziri wa Nishati na Madini William Ngeleja akijibu maswali kutoka kwa wabunge juu ya ufanyaji wa tathmini na ulipaji wa fidia kwa wananchi kutoka kwa makampuni yanayofanya utafiti wa madini ya dhahabu nchini wakati wa kipindi cha maswali na majibu leo mjini Dodoma.



Waziri mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mizengo Pinda (kulia)akijadili jambo na Waziri Ofisi ya Rais ,Utawala Bora Mathias Chikawe ndani ya ukumbi wa bunge mjini Dodoma.



Wabunge wakiwa katika kipindi cha maswali na majibu ndani ya mkutano wa wa tatu wa kikao cha kwanza cha bunge leo mjini Dodoma.(Picha na Aron Msigwa – MAELEZO).




Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Anne Makinda akitoa ufafanuzi kwa wabunge kuhusu kanuni za uendeshaji wa shughuli za bunge leo mjini Dodoma.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...