Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Saturday, July 16, 2011

WAHARIRI WAPOKEA VYETI VYAO BAADA YA KUMALIZIKA KWA MKUTANO WA JUKWAA LA WAHARIRI ARUSHA


Mzee Salim Said Salim mwandishi mkongwe kutoka Zanzibar wa tatu kutoka kulia katika picha akiwachekesha meza kuu ya JUKWAA LA WAHARIRI, mara baada ya kumaliza shughuli ya kugawa vyeti katika mkutano wa jukwaa la wahariri unaomalizika leo jijini Arusha, kulia ni Mkurugenzi wa Mawasiliano Serengeti Breweriers Tedd Mapunda, Nevile Meena Katibu wa jukwaa la wahariri, kushoto ni Theophil Makunga mjumbe wa Jukwaa la Wahariri na Mhariri mtendaji wa Mwananchi Communication na Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Absalom Kibanda na Mhariri wa Tanzania Daima. Leo baada ya kumaliza mkutano huo wahariri hao watakwenda mjini moshi ambapo watatembelea kiwanda kipya cha bia cha Serengeti Breweriers, baadae watakuwa na mchezo wa mpira wa miguu kati yao na wafanyakazi wa kampuni ya bia ya Serengeti ,na baadae watakwenda kushuhudia tamasha la Serengeti Fiesta litakalofanyika kwenye uwanja wa Ushirika Moshi leo jioni.
Theophil Makunga mjumbe wa Jukwaa la Wahariri na Mhariri mtendaji wa Mwananchi Communication, akipokea cheti chake kutoka kwa Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Serengeti (SBL)mara baada ya kumalizika kwa mkutano wa jukwaa la wahariri.
Mhariri wa gazeti la Spotstarehe Masoud Sanane akipokea cheti chake.
Mhariri wa gazeti la michezo la Bingwa Grace Hoka akipokea cheti chake.
Mhariri wa gazeti la mtanzania Dani Mwakiteleko akipokea.
Mhariri wa gazeti la Mwanahalisi Jabir Idrissa akipokea cheti chake
Deodatus Balile kutoka New Habari akipokea cheti
Mbaku Mnaku kutoka Busness Time akipokea cheti chake.
Ima Mbuguni kutoka Busnes Time akipokea cheti.
Reginand Simon kutoka mwananchi akipokea cheti.
Scolastica Mazula kutoka Times Radio akipokea cheti.
Abdallah Majura kutoka Sports FM akipokea cheti.
George Njogopa mwakilishi wa Dautch velle Sauti ya Ujerumani akipokea cheti.
John Solombi kutoka BBC akipokea cheti.
Flora Wingia kutoka Gauardian akipokea cheti.
http://fullshangwe.blogspot.com/

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...