Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Tuesday, September 13, 2011

CUF WAZINDUA KAMPENI IGUNGA LEO HUKU WAKITOA UJUMBE MZITO KUHUSU TINDIKALI


" HATUMWAGII TINDIKALI KAMA WAO" moja wa wafuasi wa CUF akiwa na bango linalosomeka hivyo, wakati wa maandamano ya kumpokea Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba ambaye baadaye alizindua kampeni za chama hicho katika viwanja vya kumbukumbu ya Samora mjini Igunga mkoani Tabora. Wiki iliyopita mfuasi mmoja wa CCM alimwagiwa tindikali na watu wasiojulikana hata hivyo kumekuwepo kushutumiana kati ya vyama vya CCM na CHADEMA kuhusiana na tukio la kinyama lililotokea Jimboni Igunga.
Mwenyekiti wa CUF Profesa Ibrahim Lipumba akiwa na mgombea Ubunge wa chama hicho Leopold Mahona kwenye mkokoteni wa punda na katika maandamano ya wanachama kwenda katika viwanja vya kumbukumbu ya Sokoine mjini Igunga kwenye uzinduzi wa kampeni za chama hicho.
Profesa Lipumba akizungumza jambo na mgombea ubunge wa chama cheke, Leopold Mahona.
."IGUNGA 'HATUTAKI VITA" mmoja wa wafuasi wa CUF (kushoto) akiwa na bango linalosomeka hivyo, wakati wa maandamano ya kumpokea Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba ambaye baadaye alizindua kampeni za chama hicho katika viwanja vya kumbukumbu ya Samora mjini Igunga mkoani Tabora.
Mlinzi wa CUF (kulia) akiwa kazini wakati wa mkutano wa uzinduzi wa kampeni za chama hicho .

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...