Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Tuesday, September 13, 2011

SEMINA YA WANAHABARI KUFANYIKA ARUSHA NA MOROGORO


Maandalizi kuhusiana na semina ya waandishi wa habari za michezo iliyopangwa kufanyika Septemba 25/25 mwaka huu mkoani Morogoro yanaendelea vizuri.

Sekretarieti ya TASWA itakutana Jumatano Septemba 14 jijini Dar es Salaam kuteua majina ya washiriki wa semina hiyo na ile itakayofanyika mkoani Arusha Oktoba 15/16 mwaka huu.

Tunaamini waandishi walio wengi watakuwepo kwenye semina hizo ama ya Morogoro au ya Arusha, isipokuwa wahariri wa habari za michezo ambao utaratibu unafanyika ili nao ifanyike ya kwao muda mfupi baada ya kumalizika semina ya Arusha.

Sekretarieti baada ya kuteua majina hayo itawasiliana na wahariri ambao waandishi wao wameteuliwa ili kupata maoni yao kwa vile uteuzi wa awali unaonesha baadhi ya vyombo wapo zaidi ya watatu, hali ambayo inaweza kuathiri utendaji wa chombo husika, lakini kama Mhariri akibariki uteuzi TASWA haitakuwa na tatizo.

Hivyo Alhamisi Septemba 15/2011, viongozi wa TASWA watafanya mkutano na wanahabari kwenye hosteli za Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), saa tano kamili asubuhi kutangaza mdhamini wa semina ya Morogoro na majina 40 ya washiriki. Wote nawakaribisha.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...