Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Friday, February 24, 2012

MAKAMU WA RAIS DKT BILAL AZINDUA MAGHARALA MAWILI YA KUHIFADHIA BIDHAA KTK BANDARI YA KASANGA NA KUTEMBELEA WAFANYA BIASHARA WA SAMAKI


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiweka Jiwe la Msingi katika moja ya jengo kati ya mawili ya Maghala ya kuhifadhia Bidhaa yaliyopo katika Bandari ya Kasanga, kijiji cha Lusambo Wilaya ya Sumbawanga, wakati akiwa katika ziara yake ya Mkoa wa Katavi na Rukwa jana februari 23, 2012.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiongozwa na Luteni Godfrey Semiono (Mkuu wa Kambi) kukagua kikosi cha Ulinzi wa Mipaka cha Kasanga kilichopo katika kijiji cha Lusambo, pembezoni mwa Wilaya ya Sumbawanga, wakati alipofika eneo hilo kwa ajili ya kuzindua maghala ya kuhifadhia bidhaa katika Bandari ya Kasanga jana Februari 23, 2012, wakati akiwa katika ziara yake ya mkoa wa Katavi na Rukwa. Picha na Muhidin Sufiani-OMR
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akitembelea kukagua maeneo ya kufanyia biashara ya baadhi ya wafanyabiashara wa samaki katika Soko la Samaki la Kasanga, baada ya kuweka jiwe la msingi katika soko hilo akiwa katika ziara yake ya Mkoa wa Katavi na Rukwa, jana Februari 23, 2012. Picha na Muhidin Sufiani-OMR
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akitembelea kukagua maeneo ya kufanyia biashara ya baadhi ya wafanyabiashara wa samaki
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisalimiana na kuwaaga wananchi wa Kijiji cha Lusambo waliojitokeza katika mapokezi yake alipofika kuweka jiwe la msingi katika Soko la Kasanga, akiwa katika ziara yake ya Mkoa wa Katavi na Rukwa jana februari 23, 2012. Picha na Muhidin Sufiani-OMR

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...