Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Monday, February 27, 2012

Ujio wa kipindi kipya cha TV "Ongea na Janet Tv Talk Show."!



Janet akirekodi kipindi na mmoja wa wadau wake aliyefika studio



Mtayarishaji wa kipindi cha Ongea na Janet TV talk show pichani kulia akiwa na mmoja wa mwanasumbwi hapa nchini Japhet Kaseba akifanya nae mahojiano kwenye moja ya kipindi chake.

Mtayarishaji wa kipindi cha Ongea na Janet TV Talk Show pichani kulia akiwa na mmoja wa wadau akifanya nae mahojiano kwenye moja ya kipindi chake.




Ongea na Janet ni Talk show ambayo inazungumzia mambo yanayotugusa katika maisha yetu ya kila siku,Inahusisha Jinsia zote na rika zote. Kipindi changu nilikitengeneza mwaka 2009 june 26 lakini bahati mbaya ilikuwa ni ngumu sana kupata airtime hasa ikizingatiwa ni kipindi toka nje ya kampuni husika,bado wahusika hawajakubali kubadilika ila hii "ishu" digital itasaidia sana. -Sijaajiriwa na Clouds Tv bali tumeingia Mkataba kama (partiners) .





Ni kipindi ambacho sitegemei kishuke bali kitakuwa kinapanda na watu wategemee mabadiliko,nimeanzia chini napanda juu katika kuleta changamoto,Natamani watu wenye talents wazitumie bila kuogopa na wasikate tamaa,kwa mfano,nimehangaika na kipindi changu kwa miaka mitatu na sasa ndio naanza kuona matunda ya uvumilivu,ubishi wa kutimiza ndoto na kutokukubali kushindwa kufikia malengo.





Wasijali maneno ya watu ya kukatisha tamaa,mtu asimame kwenye anachokiamini na akifanyie kazi haijalishi itachukua muda gani.Nategemea,kuelimisha,kushauri na kuburudisha.Niliacha kazi ITV 2008, alafu nikajiunga NGO ya Canada lakini damu yangu iko kwenye media...nimeamua kurudi na kuacha kila kitu nyuma. Nataka kukamilisha ndoto zangu zote zilizosimama kwa miaka 4.-Kipindi kinaanza tarehe 8 March,alhamis saa 3 kamili




Asanteni sana Wadau.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...