Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Saturday, March 31, 2012

Tuzo Za Wanahabari Bora



Rais Dk. Jakaya Rais wa T-anzania Jakaya Kikwete akiwa amewasili ukumbini tayari kwa kukabidhi tuzo hizo za waandishi Ijumaa usiku hapa katika picha akionekana kufuatilia ngoma ya asili kutoka kundi la Simba Theatre la jijini Dar es salaam. kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa Baraza la habari Tanzania (MCT) Chande Omar na katikati ni Katibu Mtendaji wa Baraza la Habari Kajubi Mukajanga nao wakifuatilia burudani hiyo.


Leo ndiyo leo kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee ambapo kunafanyika hafla kubwa ya utoaji wa tuzo ya Umahili wa uandishi wa habari kwa mwaka wa 2012 zinazoandaliwa na Baraza la Habari MCT na washirika wake ambapo mgeni rasmi ni Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dr. Jakaya Kikwete.





Wamejitokeza wageni waalikwa mbalimbali wakiwemo wasomi na waandishi wa habari wakongwe kama picha ya kwanza inavyoonekana kutoka kulia ni Profesa Aisha Yahya Othman mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Mlimani, Jenrrali Ulimwengu, Jaji Mstaafu Thomas Mihayo aliyesimama na Profesa Shivji kutoka Chuo Kikuu cha Dar es salaam wakiwa katika hafla hiyo usiku huu.


Hawa ni miongoni mwa majaji kulia ni Itillio Tagalile, Afisa Uhusiano wa Tanesco Badra Masoud na Wenceslaus Mushi wakijadili jambo.


Kushoto ni Awaichi Mawala kutoka Zantel na Mkurugenzi Msaidizi wa CCBRT Haika Mawala


Wageni waalikwa kutoka mashirika mbalimbali nao wamehudhuria katika hafla hiyo.


Majaji wakiwa katika meza yao.


Mwenyekiti wa bodi ya TANAPA Modestus Lilungulu kushoto na mjiumbe wa bodi Dk.Marcelina Chijoriga kulia wakiwa katika hafla hiyo.


Waziri wa habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dk. Emmanuel Nchimbi akizungumza na Katibu mtendaji wa Baraza la Habari MCT Kajubi Mukajanga.


Mhariri kutoka magazeti ya Uhuru na Mzalendo Jaquiline Liana akizungumza na Mkurugenzi wa Gazeti la Jambo Leo Juma Pinto kulia.


Clement Mshana Mkurugenzi wa Shirika la Utangazaji TBC akizungumza na Profesa Helmasi Mwansoko Mkurugenzi wa Utamaduni Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo.


Wadau kutoka Shelutete kutoka TANAPA na Geofrey Tengeneza kutoka TTB nao wapo katika hafla hiyo.



Wanaharakati kutoka taasisi mbalimbali nao wamejongea katika hafla hiyo.


Kutoka kulia ni Mbunge wa Kondoa Kusini akiwa katika picha ya pamoja na Mkurugenzi wa Michezo kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Leonard Thadeo.


Mkurugenzi wa Mawasiliano wa kampuni ya bia ya Serengeti Teddy Mapunda akiwa katika picha ya pamoja na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji na Mkurugenzi wa Fedha wa Kampuni ya bia ya Serengeti Graham Anderws


Bendi ya Msondo ikitumnuiza katika hafla hiyo.


Mzee wa Kammbi popote Antonio Lugas akiwa na mdau Abel Onesmo kutoka Clouds FM(picha zote na FullShangwe )

Katibu wa jukwaa la wahariri Tanzania Nevelin Meena aula tuzo ya habari za utawala bora ,gazeti la Uhuru latoa mpiga picha bora , majira mchora katuni bora , ITV yachukua tuzo ya habari utawala bora upande wa radio Noel Thomson aula, wateule wa magazeti habari za Maralia ni gazeti la Rai ,upande wa radio katika Maralia ni TBC ,upande wa magazeti ni IMani Imani .

Tuzo za michezo ni radio ni Abdala Machura kwa upande wa TV KIbanda amtabiria Bw.Annual Mkama afuta matokeo

Upande wa magazeti ni David Azaria wa gazeti la Habari leo kaibuka Mshindi wa habari za walemavu upande wa TV ni Lekoko Livilala upande wa Radio ni walioshindana ni Mliamani Radio na TBC one Tuma Dandi aibuka kidedea kutetea walemavu wenzake ,Nasra Abdala Kutoka gazeti la Tanzania Daima kashinda tuzo ya habari ya jinsia

Tuzo habari ZA UKIMWI katika magazeti imechuliwa na Elias Msuya kutoka gazeti la Mwananchi ,katika radio ni Betrice Nangawe kutoka radio Sun ,upande wa tuzo ya afya upande wa magazeti tuzo imekwenda kwa Sharifa Kalokola kwa upande wa radio ni Secelia Ndamakigezi ,tuzo ya mazingira kwa upande wa magazeti imechukuliwa na Lukas Liganga tuzo ya habari uchumi na biashara imekwenda kwa Bw Mashira upande wa TV ni zawadi imekwenda TBC kwa kuchukuliwa na Aneth Andwer .

Tuzo ya habari za Elimu kwa magazeti kwa Erick Kabembera upande wa TV imekwenda kwa TBC Dodoma kwa Bi. Victoria Patrick kwa upande wa radio tuzo imekwenda kwa Grece Kihondo ,tuzo ya habari wa watoto katika magazeti imekwenda kwa Nashon Kenedy ,upande wa TV ni Anganile Mwakanjala wa TBC amekuwa pekee.
Upande wa Radio tuzo ya watoto imekwenda kwa Sempaka Mchome

Tuzo ya hifadhi ZA Taifa katika magazeti imekwenda kwa Paul Jems kwa upande wa Radio imekwenda kwa TBC Taifa kwa Alex Magwesa ,huku tuzo ya utalii wa ndani upande wa magazeti imekwenda kwa Monica LUhondo awapiku Kalulunga na Midelo ,upande wa TV ni Juma Lugasi upande wa radio hakuna mshindi.

Tuzo ya maafa na migogoro katika magazeti ni Daniel Mbega ,katika TV ni Joseph Bula ambaye habari zake mbili zote ziliingia katika shindano hilo tuzo ya sayansi na Teknolojia imekwenda kwa Benard Lugongo kwa upande wa gazeti na radio ni Abel Mwende wa Claus Fm akosa mpinzani na kwa magazeti ni Nevelin Meena kwa TV hakuna Mshindi .

Tuzo ya habari zanye mvuto kwa watu upande wa magazeti ni P. Machira kwa upande wa habari za michezo na burudani upande wa TV ni Anual Mkama wa Mlimani TV akosa mpinzani ,

Kwa upande wa washindi wa jumla tuzo imechukuliwa na Nevelin Meena wa Mwananchi akabidhiwa tuzo na Rais Jakaya Kikwete aibuka na kitita cha kufa mtu dola kasha za kujiendeleza Masomo zatolewa kwake .wakati tuzo ya maisha ya mafanikio katika maisha katika tasinia ya habari imechukuliwa na Philip Karashan aliyejipatia shilingi milioni 10

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...