Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Tuesday, April 17, 2012

FABIAN JOSEPH,MARTIN SULLE,STEPHANO HUCHE WANG’ARA MASHINDANO YA NGORONGORO MARATHON YALIYOZAMINIWA NA TIGO



Fabian Joseph akihojiwa na mtangazaji wa radioFive muda mfupi baada ya kumaliza mbio za kilometa 21 za Ngorongoro Marathon zilizotimua vumbi mjini Karatu mwishoni mwa wiki.

Mshindi wa nne wa mbio za Ngorongoro Marathon,Failuna Abdi akisaidiwa kutembea baada ya kushindiwa kutembea.

Mwanariadha maarufu nchini,Restuta Joseph akihojiwa muda mfupi baada ya kumaliza mbio za Ngorongoro Marathon ziizofanyika mwishoni mwa wiki mjini Karatu mkoani Arusha
.mshindi wa kwanza wa mbio za kilometa 21 za Ngorongoro Marathon,Jacklin Sakilu akimaliza mbio zake i kwenye uwanja wa mazingira bora mjini Karatu mwishoni mwa wiki.

Washiriki wa mbio za kilometa 21 za Ngorongoro Marathon wakijiandaa kutimua vumbi kwenye lango kuu la Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro mwishoni mwa wiki.
wanariadha wakitimua vumbi kwenye mbio za Ngorongoro Marathon mwishoni mwa wiki mjini Karatu (picha zote na Charles Ndagula)

Na Charles Ndagulla,Karatu.
WANARIADHA wa maarufu nchini wanaojiandaa kufuzu kwa mashindano ya Olimpiki mapema julai mwaka huu,jana waling’ara vilivivyo katika mbio za Ngorongoro Marathon yaliyozaminiwa na Kampuni ya Tigo, baada ya kushika nafasi za juu katika mashindano hayo ya kilomita 21.
Mashindano hayo yanayondaliwa na Kampuni ya wakala wa Utalii ya Zara ya mjini Moshina kudhaminiwa na kampuni ya simu za kiganjani ya Tigo,yalishirikisha wanariadha wapatao 107 na yalianzia kwenye lango kuu la kuingia watalii la Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro na kumalizikia kwenye uwanja wa mazingira bora katika mji wa karatu.
Kwa upande wa wanaumme,Fabian Joseph alishika nafasi ya kwanza akitumia muda wa 1:03:47 huku nafasi ya pili ikikamatwa na Martin Sulle aliyetumia muda wa 1:04:26 wakati Stephano Huche mshindi w tatu wa Kilimanjaro Marathon mwaka jana akishika nafasi ya tatu kwa kutumia muda wa 1:04:30.
Mwanariadha Damian Chopa alishika nafasi ya nne kwa kutumia muda wa 1:05:05 wakati mwanariadha Pascal Momba alikamata nafasi ya tano baada ya kutumia muda wa saa 1:05:49.
Kwa upande wa wanawake,Jaklin Sakilu kutoka JWTZ Arusha alishinda mbio hizo baada ya kutumia muda wa 1:16:01 huku nafasi ya pili ikikamatwa na mwanariadha mkongwe nchini,Restuta Joseph aliyetumia muda wa 1:18:28.
Restuta kama ilivyo kwa Fabian pia anatumia mashindano hayo kujiandaa kufuzu kwa mshindano ya Olimpiki wakati mwanariadha Samson Ramadhan na Zakia Mrisho wakiwa tayari wameshafuzu.
Nafasi ya tatu kwa upande wa wanawake ilikamatwa na Siata Romanus pia kutoka JWTZ Arusha aliyetumia muda wa s aa 1:20:30 wakati Failuna Abdi msichana mdogo mwenye umri wa miaka 19 akikamata nafasi ya nne kwa kutumia saa 1:21:01 na Natali Elisante akikamata nafasi ya tano kwa kutumia muda wa saa 1:21:30.
Mbio hizo za Ngorongoro Marathon ambazo kwa sasa zimedumu kwa mwaka wa tano,zimekuwa mahususi kwa ajili ya kutoa ujumbe kwa jamii juu ya kupambana na ugonjwa wa malaria.
Mshindi wa kwanza kwa upande wa wanaume alipata zawadi ya pesa taslimu sh,500,000 huku wa pili akizawadiwa sh,300,000 na mshindi wa tatu akipewa sh,150,000 huku kwa upande wa wanawke mshindi wa kwanza akilamba 300,000,wa pili 150,000 na wa tatu akipata sh,100,000.
Akizungumza mara baada ya mbio hizo,kocha wa Taifa wa Riadha,Zacharia Gwandu alisema kuwa mwanariadha Dixon Marwa ambaye hakushiriki mashindano hayo,anajindaa na marathon ya kufuzu Olimpiki April 29 mwaka huu huko Harmburg nchini Ujeruman.
Kwa upande wake Fabian,kocha huyo alisema kuwa,anatazamiwa kushiriki marathon ya kufuzu kwa Olimpiki Mei 13 mwaka huu katika mji Mkuu wa Jamhuri ya watu wa Zcheck wa Prague.
Alisema kwa ujumla hali ya kambi iliyopo Kibaha mkoani Pwani ni nzuri na kwamba wanariadha wote wamekuwa wakihudumiwa vizuri na kwamba kambi hiyo imeanza wakati mwafaka.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...