Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Wednesday, May 30, 2012

Meneja mkuu wa kampuni ya tigo atembelea kampuni ya Clouds Media Group leo jijini Dar


Meneja Mkuu wa kampuni ya simu ya mikononi ya Tigo,Diego Gutierrez akizungumza jambo kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Clouds Media Group,Joseph Kusaga pichani kulia,mara baada ya kumaliza ziara ndani ya kampuni hiyo  na kujionea mambo mbalimbali,shoto ni Ofisa Mahusiano wa Tigo Alice Maro.
 Meneja Mkuu wa kampuni ya simu za mikononi ya Tigo akifanya mahojiano mafupi na mtangazaji wa Choice FM,aitwaye Thandi Kathembe mapema leo jioni.
Mkuu wa Vipindi wa Clouds FM,Sebastian Maganga (pili kutoka kulia),akifafanua jambo kwa Meneja Mkuu wa kampuni ya simu ya mikononi ya Tigo,Diego Gutierrez alieambatana na Ofisa Mahusiano wake, Alice Maro,kulia ni Dj Fetty.
Mkuu wa Vipindi wa Clouds FM,Sebastian Maganga akifafanua jambo kwa Meneja Mkuu wa kampuni ya simu ya mikononi ya Tigo,Diego Gutierrez (pichani kati),Kulia ni mmoja wa watangazaji wa Clouds FM,Ruben Ndege.
Meneja Mkuu wa kampuni ya simu ya mikononi ya Tigo,Diego Gutierrez akiperuzi moja ya jarida la Burudani hapa nchini la KITANGOMA,linalochapishwa na kampuni ya Prime Time Promotions LTD. 
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Clouds Media Group,Joseph Kusaga akimuelekeza Meneja Mkuu wa kampuni ya simu ya mikononi ya Tigo,Diego Gutierrez namna ya baadhi ya vipindi vya Clouds TV vikiwa tayari kwa kurushwa hewani.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Clouds Media Group,Joseph Kusaga akimuelekeza Meneja Mkuu wa kampuni ya simu ya mikononi ya Tigo,Diego Gutierrez namna ya baadhi ya vipindi vya Clouds TV vikitayarishwa kabla ya kwenda kurushwa hewani.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...