Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Monday, June 4, 2012

Benki ya CBA kuwanufaisha wateja wake


Na Philemon Solomon wa Fullshangwe-Dar es salaam
 
BENKI ya Commercial of Africa Tanzania Limited imeanzisha promosheni ambapo wateja wake watanufaika na zawadi mbalimbali.
Akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Mkuu wa Kitengo cha wateja binafsi wa Benki hiyo, William Mungai alisema promosheni hiyo itasaidia kuboresha maisha ya wateja wao na wafanyakazi wa benki hiyo.
Alisema promosheni hiyo kwa mwezi itahusisha makampuni, wateja binafsi ambapo mteja atatakiwa kufungua akaunti mpya kwa kiwango cha chini cha milioni 50 ataingia kwenye droo ya kujishindia Laptop.
Alisema mteja akiweka pesa marambili zaidi kwenye akaunti yake ya Current kwa kiasi kisichopungua milioni 20 naye ataingia kujishindia Laptop.
"Mteja atakaye mshawishi mshirika wake mfanyabiashara, SME, Msambaji, rafiki kufungua akaunti kwa kiasi kisichopungua milioni 15 ataingia kwenye droo ya kujishindia kompyuta ya mezani''. alisema Mungai.
Aliongeza kuwa watu wote watakaokidhi vigezo cha kwanza na cha tatu wataingia kwenye droo kubwa ya kushinda kompyuta na printa.
Alisema kwa wateja binafsi wanapaswa kufungua akaunti mpya kwa kiwango cha chini cha milioni 1 na kuiongia kwenye droo ya kujishindia Tv ya Plasma.
Alisema mteja akiweka fedha zaidi ya mara mbili katika akaunti yake kwa kiasi kisichopungua sh. milioni 500 ataingia kwenye droo ya kujishindia DVD Home Theater.
Alisema kwa mtu atakaye mshawishi rafiki, mshirika na kufungua akaunti ya familia yaani mke na mtoto mmoja kwa kiasi kisichopungua sh. milioni 1 ataingia kwenye droo ya kujishindia TV ya Plasma.
Alisema kwa wateja watakaoingia robo mwaka ambapo itakuwa ni mwisho wa kampeni na kukithi vigezo namba moja na tatu wataingia kwenye droo kubwa ya kushinda Friji, DVD Home Theater na TV Plasma.
Alitoa mwito kwa waqnanchi kufungua akaunti mpya, kuweka fedha mara mbili au kumshawishi mtu au kampuni kufungua akaunti ili kushinda zawadi hizo.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...