Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Sunday, June 17, 2012

MBUNGE WA SINGIDA MJINI MOHAMED DEWJI ATOA MSAADA WA PIKI PIKI JIMBONI


Mbunge wa jimbo la Singida mjini Mh. Mohammed Gullam Dewji akizungumza na wafanyabiashara wa bodaboda (hawapo kwenye picha) muda mfupi kabla hajawakabidhi msaada wa pikipiki kumi zenye thamani ya shilingi milioni 20.Kushoto ni katibu wa umoja wa wafanyabiashara wa bodaboda, Maulid Mpondo.Kulia wa kwanza ni Kaimu mkurugenzi wa manispaa ya Singida,Williamu Haaly na anayefuata,ni katibu wa CCM manispaa ya Singida.


Mbunge wa jimbo la Singida mjini Mh. Mohammed Gullam Dewji akimkabidhi katibu wa umoja wa wafanyabishara wa bodaboda msaada wa pikipiki 10.
Pikipiki 10 aina ya sanlag CC150 zilizotolewa msaada ya mbunge wa jimbo la Singida mjini, Mohammed Gullam Dewji kwa vikundi 10 vya wafanyabiashara wa bodaboda mjini Singida.

Baadhi ya wafanyabiashara wa bodaboda wa mjini Singida wakiserebuka na kucheza 'KIDUKU' na mbunge wao Mohammed Gullam Dewji muda mfupi kabla ya mbunge huyo kuwakabidhi wafanyabiashara hao msaada wa pikipiki.



Na Geofrey Mwakibete na Nathaniel Limu
Wafanyabiashara wa bodaboda jimbo la Singida mjini,wamehimizwa kuunda/kuanzisha vikundi ili pamoja na mambo mengine, kujijengea mazingira mazuri ya kukopesheka.
Wito huo umetolewa na mbunge wa jimbo la Singida mjini,Mohammed Gullam Dewji,wakati akizungumza kwenye hafla iliyofana, ya kukabidhi pikipiki 10 aina ya sanlag CC 150 zenye thamani ya shilingi milioni 20 kwa vikundi vya wafanyabiashara wa bodaboda.
Alisema faida za kujiunga kwenye vikundi ni nyingi ikiwemo ya kuwa nafasi nzuri ya kupata mikopo mbalimbali kutoka kwenye taasisi za kifedha.Mtu mmoja mmoja akitaka kukopa fedha benki ni ngumu, kuotokana masharti yaliyowekwa na taasisi za kifedha.
“Siku zote umoja ni nguvu,utegano unachangia kuleta ulegevu unaozaa udhaifu.Mahali pana ulegevu,kwanza hakuna maendeleo ya kweli na pia kutetea haki,inakuwa ngumu mno”,alifafanua Dewji ambaye pia ni mjumbe wa NEC CCM mkoa wa Singida.
Kuhusu pikipiki hizo alizotoa msaada, alisema lengo lake ni kwamba kila kikundi kitaitumia pikipiki yake kwa ajili ya kukiongezea kikundi mapato ambayo endapo yatatunzwa vizuri,ipo siku kila mwanakikundi anaweza akamiliki pikipiki yake binafsi.
Aidha, amewataka wakati wote kuzingatia sheria halali zilizowekwa na mamlaka husika, ili shughuli zao ziweze kuendelea bila matatizo.
“Pia napenda kutumia fursa hii, kuomba mamlaka zinazohusika na sheria za usalama barabarani na utozaji wa kodi na ushuru, kujipanga kwa ajili ya kutoa elimu kwa wafanyabiashara wa bodaboda,ili waweze kuzifahamu sheria husika”,alisema na kuongeza;
“Nina imani kwamba wafanyabiashara wa boda boda wakifahamu kwa kina sheria za usalama barabarani,kutapunguza mno ajali na pia wakifahamu mambo ya kodi na ushuru,hawatakwepa kulipa”.
Katika hatua nyingine, Dewji amewahimiza waumini wa madhehebu ya dini, kuongeza kasi ya utoaji sadaka,ili kuimarisha ustawi wa madhahebu yao.
Alisema waumini wanao wajibu mkubwa wa kuchangia kwa hali na mali madhehebu yao kwa lengo yaweze kutekeleza wajibu wake kwa ufanisi zaidi.
“Sadaka inayotolewa kwa moyo mkujufu,licha ya kusaidia ustawi wa dhehebu la dini husika,mtoaji anakuwa amejiwekea thawabu mbele ya mwenyezi Mungu”,alisema Dewji.
Akiijengea nguvu hoja yake hiyo,mbunge huyo, alisema ustawi wa kweli wa dhehebu la dini,utaletwa na waumini wenyewe,watu wengine/taasisi zingine,kazi zao ni kusaidia mahali waumini wanapokuwa wamepelea.
Katika siku yake ya pili ya ziara yake ya kikazi jimboni kwake,Dewji alitoa msaada wa mifuko ya saruji 40 kwa msikiti wa kijiji cha Manguamitogho na mifuko mingine 25 ya saruji na shilingi laki tano taslimu, kwa kanisa la Pentekoste la kijiji cha Ititi.
Katika siku yake ya mwisho ya ziara yake (17/6/2012),Dewji alitarajiwa kuwa na kikao maalum na madiwani wa kata za Singida mjini,kuzindua kisima cha maji cha kijiji cha Mtisi,kuzungumza na wanachama wa klabu ya waandishi wa habari mkoa wa Singida na kukagua kituo cha afya cha Sokoine mjini Singida

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...