Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Tuesday, June 19, 2012

MWENYEKITI ATUHUMIWA KUHUJUMU BODI YA MAJI




 
NA GLADNESS MUSHI WA FULLSHANGWE-ARUSHA
 
MWENYEKITI wa CCM kata ya Olturument,Thelesia Kitalu anatuhumiwa kuihujumu bodi ya maji ya kata hiyo,(Meviwasu) kwa kuhamasisha wananchi kungóa mita za maji zinazofungwa kwenye makazi yao, sanjari na kukata mabomba ya maji na kujiunganishia kinyemela akiwaeleza kuwa maji hayo ni ya bure na haifai kuyalipia .

Pia anadaiwa kufadhili kikundi cha vijana 12 wanaotambulika kwa jina la ‘’Talban’’,ambao wamekuwa na kazi moja ya kungóa mita za mabomba majira ya usiku na kuendesha vurugu kwa kuwapiga wafanyakazi wa Meviwasu ,wakipinga hatua ya kulipa maji hayo kwa bill huku akiwaeleza wananchi kuwa shirika la Meviwasu linalojihusisha na mradi wa usambazaji wa maji vijijini, halipo kisheria.
Add captionHayo yalibainika jana kati ka mkutano mkuu wa dharura wa bodi ya maji (Meviwasu)uliofanyika katika kijiji cha Ilkishini wilaya ya Arumeru,uliowahusisha viongozi wa kitongoji ,kijiji na kata,madiwani ,askari polisi pamoja na wazee mashuhuri kutoka vijiji sita vinavyohudumiwa na shirika la Meviwasu .

Akizungumza katika mkutano huo mwenyekiti wa bodi ya maji ,Lomayani Meshurie alisema kuwa lengo la mkutano huo wa dharura ni kujadili hujuma ya ungóaji wa mabomba na mita za maji unaoendelea,ambapo alielekeza lawama moja kwa moja kwa mwenyekiti huyo wa ccm anayedaiwa kuwashawishi wananchi wasikubali kuwekewa mita ili walipie huduma ya maji safi.

Baadhi ya viongozi wa vijiji na vitongoji waliunga mkono hoja hiyo na kuthibitisha wazi kuwa mwenyekiti huyo wa ccm ndiye amekuwa akitumia mikutano yake ya hadhara kuwashawishi wananchi waukatae mradi huo wa maji ,akidai shirika hilo la Meviwasu ambalo limetokana na muunganiko wa vijiji viwili vya Muklat na Enaboishu haliko kisheria.

Shirika la Meviwasu limekuwa likiendesha mradi huo wa maji kwa vijiji saba vilivyomo wilayani Arumeru,chini ya ufadhili wa shirika la ( Ubu) la nchini Denmack linalojihusisha kusaidia miradi endelevu ya maji kwa nchi zinazoendelea.

Mmoja wa wazee mashuhuri mkazi wa kijiji cha Ekenywa, Mzee Logolie Sailevu alisema kuwa mwenyekiti huyo amekuwa akihujumu mradi huo kwa lengo la kujipendekeza kwa wananchili ili kujenga mazingira ya kuchaguliwa katika nafasi ya uongozi ujao hatua ambayo imesababisha kukwama kwa zoezi la usambazaji maji kwa wananchi.

‘’huyo mama achukuliwe hatua kali hapa tunao askari polisi ili kushughulika masuala hayo ,amekuwa akiongoza kundi la vijana wa Talban ili kungóa mita ndio maana vijiji vingi havina maji, huu mradi umeshindwa kufikia malengo kwa sababu yake ‘’alisema Mzee Logolie huku akishangiliwa

Akizungumza katika mkutano huo,mwenyekiti huyo anayetuhumiwa, alikiri kulifahamu kundi hilo la Talban na kudai kuwa si kweli kwamba analifadhili ili kungóa mita za maji ila alisisitiza kuwaamekuwa na ukaribu na kundi hilo kwa sababu wamekuwa wakimfuata na kumweleza kero mbalimbali.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...