Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Thursday, June 21, 2012

NBC YADHAMINI KIASI CHA DOLA ZA KIMAREKANI 70,000 KWA AJILI YA UTAFITI


 Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC Tanzania, Lawrence Mafuru
(kushoto) akikabidhi mfano wa hundi ya Dola za Kimarekani 70,000 kwa
waandaaji wa utafiti wa kupata makampuni bora 100 ya kati, Mkurugenzi
Mtendaji wa kampuni ya KPMG, David Gachewa (kulia) na Mhariri
Mtendaji wa Mwananchi Communications, Theopil Makunga. Hafla ya
makabidhiano imefanyika jijini Dar es Salaam leo.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC Tanzania, Lawrence Mafuru
(kushoto) akizungumza katika hafla ambyo NBC ilikabidhi hundi ya Dola
za Kimarekani 70,000 kwa ajili utafiti wa kupata makampuni bora 100 ya
kati unaoandaliwa na kampuni ya KPMG kwa kushirikiana na Kampuni ya
Mwananchi Communications. Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa KPMG
Tanzania, David Gachewa. Hafla hiyo ilifanyika jijini Dar es Salaam
leo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC Tanzania, Lawrence Mafuru
(katikati) akishikana mikono na Mhariri Mtendaji wa Mwananchi
Communications, Theopil Makunga katika hafla ambayo NBC ilikabidhi
hundi ya Dola za Kimarekani 70,000 kwa ajili utafiti wa kupata
makampuni bora 100 ya kati unaoandaliwa na kampuni ya KPMG kwa
kushirikiana na MCL. Hafla hiyo imefanyika jijini Dar es Salaam leo.
Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa KPMG, David Gachewa.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...