Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Tuesday, June 5, 2012

SUGU, VINEGA, JUMA NATURE, PROF JAY WAFUNIKA DAR LIVE


Msanii mahiri wa HIP HOP ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Mbeya Mjini (Chadema), Joseph Mbilinyi 'Mr II' a.k.a Sugu, juzi alizikonga nyoyo za mashabiki wake waliofurika ndani ya ukumbi wa Dar Live uliopo Mbagala Zakhem jijini Dar es Salaam kwa kufanya makamuzi ya hatari katika tamasha la Usiku wa Sugu. Sugu alisindikizwa na Juma Nature, Profesa Jay, Vinega, Mkoloni na wengineo wengi kwenye shoo hiyo iliyokuwa ya aina yake.
Katika picha juu Sugu akiwarusha mashabiki waliofurika ndani ya Dar Live usiku wa kuamkia leo.
Sugu na Mkoloni wakizidi kuwadatisha mashabiki.
Mbunge wa Arumeru Mashariki (Chadema), Joshua Nassari nae akitoa 'verse' kuupamba usiku wa Sugu ndani ya Dar Live.
Profesa Jay akiwapa burudani mashabiki wa Dar Live.
Juma Nature na kundi lake la Wanaume Halisi likifanya makamuzi stejini.
Suma G nae alikuwepo kuupamba usiku huo.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...