Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Wednesday, June 6, 2012

Wabunge wa Bunge la Afrika Mashariki wala Kiapo


Wabunge wa Bunge la Afrika Mashariki (EALA) leo wameapishwa rasmi kushika madaraka hayo huku Tanzania ikiwa na Wawakilishi tisa katika Bunge hulo.

Wabunge hao waliapa baada ya kupatikana Spika wa mpya wa Bunge hilo ambapo safari hii ikiwa ni Uganda kushika Uongozi huo wa Juu wa Bunge na Mwana Uchumi, Margareth Zziwa kuchukua nafasi hiyo.

Wabunge wote wa Tanzania katika Bunge la Jumuiya ya Mashariki waliokula kiapo hii leo ni pamoja na Mwenyekiti wa Wabunge wa Tanzania kwenye Bunge EALA, Alhaj Adam Omar Kimbisa na Katibu wake, Mh Shy-Rose SaddrudinBhanji.

Wengine ni Mhe. Anjela Charless Kizigha, Mh. Maryam Ussi Yahya,Mh.Nderkindo Perpetua Kessy, Dkt Twaha Issa Taslima, Mhe. Abdullah Ali Hassan Mwinyi, Mhe Bernard Musomi Murunyana Mhe. Charles Makongoro Nyerere na Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta anaeingia kwa wadhifa wake wa Uwaziri.

Wabunge hao wameapisha pamoja na wabunge wenzao wa Kenya, Uganda, Rwanda na katika picha juu ni Waziri wa Afrika Mashariki na mbunge wa Urambo Mh Samwel Sitta akiapa katika bunge hilo jana jijini ArushaSOURCE: FATHER KIDEVU BLOG
Mbunge Shy-Rose Banji akila kiapo chake
Mh. Alhaji. Adam Kimbisa
Mhe. Anjela Charless Kizigha
Mhe Bernard Musomi Murunyana
Mh.Abdullah Alli Hassan Mwinyi 
Mh.Nderkindo Perpetua Kessy
Mh.Charles Makongoro Nyerere
Dkt Twaha Issa Taslima

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...