Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Thursday, June 21, 2012

WENGI WAMUAGA MAREHEMU WILLY EDWARD KATIKA VIWANJA VYA MNAZI MMOJA



 Prof. Ibrahim  Lipumba kushoto Mwenyekiti wa chama cha wananchi CUF, Katibu wa CCM Itikadi na Uenezi Nape Nnauye, na Mwenyekiti mtendaji wa makampuni ya IPP Bw. Reginald Mengi wakijumuika pamoja na viongozi wengeni, ndugu jamaa na marafiki pamoja na waombolezaqji wengine walioudhuria katika ibada ya  kuaga mwili wa marehemu Willy Edward Ogunde aliyekuwa mhariri mkuu wa Gazeti la  Jambo leo katika viwanja vya mnazi mmoja jijini Dar es salaam jana.
(PICHA NA PHILEMON SOLOMON WA FULLSHANGWE)

Mwili wa marehemu Willy Edward Ogunde aliyekuwa mhariri mkuu wa Gazeti la  Jambo leo ukiwasili  katika viwanja vya mnazi mmoja jijini Dar es salaam jana.

Mjane wa Marehemu Willy Edward Bi Rehema akifarijiwa na ndugu huku akilia kwa uchungu kwa kumpoteza mume wake mpendwa marehemu Willy Edward.
Mwenyekiti wa IPP Reginald Abraham Mengi, Akimfariji Athumani Hamisi katika msiba huo
Mwenyekiti wa makampuni ya  IPP Reginald Abraham Mengi, Akitoa heshima zake za mwisho kwa mwili wa marehemu Willy Edward wanaofuatia nyuma yake ni Mwenyekiti wa CUF Prof. Ibrahim Lipumba na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM Nape Nnauye
Baadhi ya waombolezaji walioudhuri katika kuuaga mwiliwa marehemu Willy Edward wakiwa katika mstari tayari kwa kutoa heshima zao za mwisho kwa marehemu.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...