Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Tuesday, June 5, 2012

ZANZIBAR HEROES YAUA 6-0 KOMBE LA DUNIA



Kikosi cha Zanzibar Heroes
TIMU ya soka ya taifa ya Zanzibar, Zanzibar Heroes imeanza vyema mchezo wake wa kwanza wa mashindano ya VIVA world Cup uliochezwa jana saa 4 usiku katika uwanja wa Francios Harir ndani ya jiji la Ebril, Kurdistan kwa kuwabamiza bila huruma timu ya Ratia kutoka bara la Ulaya mabao 6 -0.
Heros walicheza kwa umakini mkubwa katika dakika 20 za kwanza, wakijaribu kuusoma mchezo. Iliichukua Heroes dakika 33 kupata bao la kwanza lililofungwa na Khamis Mcha (Viali) ambae katika mchezo huo amefunga ha-trick. Mabao mengine mawili aliyafunga katika dakika ya 41 na 57.
Wafungaji wengine wa heroes walikuwa ni Abdi Kassim (Baby) dakika ya 51, Awadh Juma alieingia kipindi cha pili aliifungia Heroes mabao 2 katika dakika za 88 na 90 za mchezo.Katika mchezo huo, Zanzibar Heroes walionekana kuelewana vyema,kuanzia nyuma, kati na safu ya ushambiliaji.
Wapenzi wengi waliodhuria walivutiwa sana na kiwango cha mpira cha Zanzibar heros, huku wakipongeza na wengine wakitabiri inaweza kufika fainali. Wachezaji wote wako na afya njema, hakuna majeruhi huku wakiwa na ari kubwa ya kuchukua kombe hilo kwa nchi wasio wanachama wa FIFA.
Katika mechi nyengine, wenyeji Kurdistan waliwashinda Western sahara kwa 6-0, na mechi ya Awali Dafur walifungwa 15 na Nothern Cyprus.
Zanzibar heroes itacheza mechi yake ya pili kesho usiku na ikishinda watajihakikishia kucheza nusu fainali

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...