Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Thursday, March 21, 2013

Kampuni za simu za mkononi zaongoza kutangaza biashara nchini



 Mkurugenzi Mtendaji wa Push Observer, Rubelyn Alcantara akizungumza wakati wa uzinduzi wa huduma hiyo katika hafla fupi iliyofanyika kwenye ofisini mwa Push Observer, Kinondoni.
 Baadhi ya maofisa kutoka makampuni mbali mbali wakielekezwa jinsi kampuni ya Push Observer inavyofanya shughuli zake kutoka kwa mmoja wa wafanyakazi wa kampuni hiyo.

Na Mwandishi wetu
KAMPUNI za mitandao ya simu za mikononi nchini zimeshika nafasi ya kwanza  katika kutangaza biashara zao kwenye vya habari nchini kwa robo ya mwisho ya mwaka jana.
Kwa mujibu wa takwimu zilizotolewa na kampuni inayoongoza katika kusimamia na kufuatilia mwenendo wa vyombo vya habari nchini, Push Observer, kampuni ya simu ya mkononi ya Airtel ndiyo inayoshika nafasi ya kwanza kwa kutangaza matangazo mengi nchini.
Mkurugenzi mtendaji wa Push Observer, Ruby Alcantara alisema kuwa kampuni ya pili ni Tigo na kufuatiwa na Vodacom Tanzani katika nafasi ya tatu na Zantel katika nafasi ya nne. Kampuni ya bia Tanzania (TBL) inashika nafasi ya tano ikifuatiwa na Pepsi, Star Times, Coca Cola, SBL na Twaweza katika nafasi ya 10.
Bi. Alcantara alisema kuwa takwimu hizo ni za uhakika kutokana na kukusanya rekodi hizo kwa kupitia vifaa  vya  kisasa walivyowekeza katika sekta hiyo.
Alisema kuwa jumla ya fedha zilizotumika kwa makampuni yote 20 bora katika kutangaza biashara ni sh  bilioni 17, 827,970, ingawa taarifa hiyo haija ainisha gharama halisi ya kila kampuni ilizotumia katika kutangaza bidhaa zake.
“ Hatuwezi kuweka bayani ni kiasi gani cha fedha kimetumika katika zoezi hili, ni vigumu kufanya hivyo, lakini takwimu zetu ni sahihi kutokana na vifaa tulivyowekeza katika kutoa huduma hii, ni ya kisasa na yenye ubora wa kimataifa, tutakuwa tunatoa taaifa hizi kila baada ya miezi mine,” alisema.
Alisema kuwa vyombo vya habari vinavyofaidika kwa kupata matangazo mengi ni redio na televisheni. Amesema kuwa kampuni yao itakuwa inatoa taarifa kuhusiana na watangazaji bora wa kwenye vyombo vya habari kila baada ya miezi mitatu. Ripoti  robo ya kwanza ya mwaka huu inatarajiwa kutolewa mwezi ujao mwanzoni.
“Ripoti hii inatoa  fursa kwa kila kampuni kujua utendaji wake katika ushindani wa kibiashara, pia kujua mshindani wako anafanya nini katika kujitangaza  na kukuwezesha kubadili mbinu ili uweze kuendeleza ushindani au kuweza kuendelea kushika nafasi ya kwanza kibiashara,” alisema.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...