Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Saturday, November 30, 2013

PIKI PIKI YA MABONDIA NASSIBU RAMADHANI NA MOHAMED MATUMLA YAONESHWA


Meneja Masoko wa kampuni ya haojue,Wawa Laida kulia akiwaonesha pikipiki itakayogombaniwa Dar es salaam jana na mabondia Nassibu Ramadhani kushoto na Mohamed Matumla siku ya Desemba 25 katika ukumbi wa friends corner wengine wa pili kushoto ni Rashidi Matumla,Christopher Mzazi na mlatibu wa mpambano uho Kaike Siraju Picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com
Mratibu wa mpambano wa ndondi Kaike Siraju akiojiwa akiwa juu ya pikipiki itakayogombaniwa na mabondia Mohamed Matumla na Nassibu Ramadhani siku ya Desemba 25 Picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com
Meneja Masoko wa kampuni ya haojue,Wawa Laida kulia akiwaonesha pikipiki itakayogombaniwa Dar es salaam jana  na mabondia Nassibu Ramadhani kushoto na Mohamed Matumla siku ya Desemba 25  wengine wa pili kushoto ni Rashidi Matumla,Christopher Mzazi na mlatibu wa mpambano uho Kaike Siraju Picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com

Meneja Masoko wa kampuni ya haojue,Wawa Laida kulia akiwaonesha pikipiki itakayogombaniwa Dar es salaam jana  na mabondia Nassibu Ramadhani kushoto na Mohamed Matumla siku ya Desemba 25  wengine wa pili kushoto ni Rashidi Matumla,Christopher Mzazi na mlatibu wa mpambano uho Kaike Siraju Picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com

Friday, November 29, 2013

MATEMBEZI YA DAR MPAKA MORO YAZINDULIWA JIJINI DAR ES SALAAM KUANZA JANUARI 11-2014


 Ni changamoto inayotolewa mbele ya Watanzania,kukumbuka maana halisi ya  uzalendo kujitoa mhanga kuweza kufanikisha maendeleo yao wenyewe kwa kujishughulisha na kujibidisha katika nyanja mbalimbali kwa manufaa ya Taifa,kujitolea kuanzia ngazi ya kaya mpaka taifa,kuacha kulalama tu kuwa serikali haijawafanyia moja ama mbili lakini wao wenyewe kutambua mchango wao kama Watanzania na wajibu wao kama wananchi, kubwa zaidi kujivunia nchi iitwayo Tanzania kwa yale mema na adimu yaliyopo na kurekebisha palipo na kasoro kwa moyo mmoja bila kujali itikadi,imani, asili ama mtizamo miongoni mwetu, Tanzania,kwa nini Dar es Salaam mpaka Morogoro.Dar es Salaam imeendelea kuwa kituo kikuu cha shughuli nyingi za kiuchumi,kiserikali na vilevile ni mkoa ulio na watu wengi zaidi Tanzania, takribani milioni mbili na nusu (2.5mil) kwa mujibu wa sensa ya watu ya mwaka 2002, wakati Morogoro ina watu wasiofika laki tatu , na kwa ukuaji wa asilimia 4.39 kwa mwaka inaweza pia kuwa ya tatu barani Afrika na tisa duniani, hii inawakilisha tofauti kubwa sio tu kwa idadi lakini ya ukuaji, upatikanaji wa huduma za msingi za kijamii, ukuaji wa kiuchumi na vilivile hali ya kipato na fursa za kiuchumi” alisema Chuma.(PICHA NA PHILEMON SOLOMON WA FULLSHANGWE DAR ES SALAAM)

Waziri Kigoda mgeni rasmi tamasha la Handeni Kwetu



Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
WAZIRI wa Viwanda Biashara na Masoko ambaye pia ndio mbunge wa Handeni, Dkt Abdallah Kigoda, anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika Tamasha la Utamaduni, lililopangwa kufanyika Katika Uwanja wa Azimio, wilayani Handeni mkoani Tanga, Desemba 14 mwaka huu.
Hon-KIGODATamasha hilo linafanyika kwa mara ya kwanza wilayani hapa, huku likitarajiwa kuwa la aina yake kutokana na maandalizi yanayoendelea kushika kasi, ambapo kwenye uwanja huo, Tamasha hilo litaanza saa 2 asubuhi hadi saa 12 za jioni.
Akizungumza jana mjini Handeni, Mratibu wa Tamasha hilo, Kambi Mbwana, alisema maandalizi yamezidi kushika kasi kwa kuangalia mazoezi ya vikundi kadhaa vitakavyotoa burudani katika tukio hilo.
“Tunashukuru Mungu kuona mambo yanazidi kuwa mazuri kwa kuhakikisha kuwa Desemba 14 mwaka huu tunafanya tamasha lenye mguso na kila mmoja wetu kufaidishwa.
 
“Huu ni wakati wa kila mtu kujipanga ili aje kushiriki kwa namna moja ama nyingine, ukizingatia kuwa juhudi hizi zote zipo kwa ajili ya kujenga ushirikiano kwa watu wote,” alisema Mbwana.
Wadhamini katika tamasha hilo ni pamoja na gazeti la Mwananchi, Clouds Media Group, ni Phed Trans, Clouds Media Group, Grace Products, Screen Masters na mtandao wao wa Saluti5.com, Dullah Tiles & Construction Ltd, Katomu Solar Specialist, PLAN B SOLUTIONS (T) LTD, Country Business Directory (CBD) na Michuzi Media Group duka la mavazi la Chichi Local Ware, Smart Mind & Arters chini ya Anesa Company Ltd, ikidhamini kwa kupitia kitabu chao cha ‘Ni Wakati Wako wa Kung’aa’, Lukaza Blog, Kajunason Blog, Jiachie Blog, Pamoja Pure Blog na Taifa Letu.com.

MTANZANIA CLARA NOOR AANZA KUNG'ARA MASHINDANO YA MISS EARTH UFILIPINO


 Mwandishi Wetu
Nyota wa mrembo wa Tanzania anayewania taji la Miss Earth, Clara Noor imeanza kung’ara baada ya kuibuka mshindi wa kwanza katika taji la fukwe ya Pagudpud iliyopo nchini Phillipines.
Mbali ya kutwaa taji hilo, Clara pia ameibuka mshindi wa tatu katika taji la vazi la Taifa na kuzipiku nchi nyingine nyingi na kuzawadiwa medali ya shaba.
Katika mashindano ya tuzo maalum, jumla ya tuzo 11 zilikuwa zinagombaniwa na warembo 88 walikuwa wanawania mataji hayo ambayo zawadi zake zilitolewa na wadhamini hao.
Clara alionyesha uwezo mkubwa katika taji hilo na kuwa mwafrika wa kwanza kushinda katika historia. Katika vazi la Taifa, Clara aliwavutia wengi na kupata ushindani mkubwa kutoka kwa mrembo wa warembo kutoka Afrika Kusini, Ashanti Mbanga na kutoka Nigeria, Marie Miller ambao walishika nafasi ya kwanza nay a pili.
Muandaaji wa Miss Earth Tanzania, Maria sarungi Tsehai alisema kuwa ni faraja kubwa kwa Clara kuitangaza Tanzania kwa kupitia mataji hayo mawili kwani mbali ya jina lake, kinachotangazwa pia ni nchi.
“Amefanya vyema mpaka sasa, tunatarajia kuona anaendelea kufanya vizuri na kutuletea sifa, mpaka sasa anastahili pongezi,” alisema Maria ambaye ni Mkurugenzi wa Kampuni ya Compass Communications.
Alisema kuwa fainali ya mashindano hayo yatafanyika Desemba 7 kwenye ukumbi wa Versailles Palace, Alabang, Muntinlupa City na kurushwa live na vituo vya televisheni vya STAR World, ABS-CBN, Velvet, The Filipino Channel, Ustream na VenevisiĆ³n.

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AWAONGOZA WAOMBOLEZAJI MAZIKO YA MTOTO WA MAKAMU MWENYEKITI WA CCM, PETER MANGULA MAKABURI YA KINONDONI


 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiweka udongo katika kaburi la mtoto wa Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara, Philip Mangula, (Peter Mangula), wakati wa shughuli za maziko zilizofanyika katika makaburi ya Kinondoni Kisutu jijini Dar es Salaam,leo.
Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara, Philip Mangula, akiweka udongo kwenye kaburi la mtoto wake, Peter Mangula, wakati wa shughuli za maziko zilizofanyika katika makaburi ya Kinondoni Kisutu jijini Dar es Salaam,leo.
 Watoto wa marehemu, wakiweka udongo kwenye kaburi ikiwa ni ishara ya kumzika baba yao.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiweka Shada la maua kwenye kaburi la mtoto wa Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara, Philip Mangula, (Peter Mangula), wakati wa shughuli za maziko zilizofanyika katika makaburi ya Kinondoni Kisutu jijini Dar es Salaam,leo.
 Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara, Philip Mangula, akiwaongoza sehemu ya wanafamilia kuweka shada la maua kwenye kaburi la mtoto wake, (Peter Mangula), wakati wa shughuli za maziko zilizofanyika katika makaburi ya Kinondoni Kisutu jijini Dar es Salaam,leo.
 Baadhi ya Vijana wa CCM, wakibeba Jeneza lenye mwili wa marehemu Peter Mangula, wakati wakiwasili kwenye makaburi ya Kisutu Kinondoni kwa maziko.
 Jeneza lenye mwili wa marehemu Peter Mangula likishushwa kaburini.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akijumuika na waombolezaji wakati wa shughuli za maziko ya mtoto wa Mwenyekiti wa CCM Bara, Philip Mangula, (Peter Mangula) zilizofanyika kwenye Makaburi ya Kisutu jijini Dar es Salaam, leo.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akijumuika na waombolezaji wakati wa shughuli za maziko ya mtoto wa Mwenyekiti wa CCM Bara, Philip Mangula, (Peter Mangula) zilizofanyika kwenye Makaburi ya Kisutu jijini Dar es Salaam, leo.
 Waziri Mkuu Mstaafu, Salim Ahmed Salim,akiwaongoza mawaziri wenzake wastaafu, kuweka mashada ya maua.
 Naibu Katibu Mkuu wa CCM Bara, Mwigulu Nchemba na Naibu Katibu Mkuu CCM Zanzibar, Vuai Ali Vuai, wakiweka mashada ya maua.
 Katibu Mkuu wa Chadema, Dkt. Wilbload Slaa, akiweka Shada la maua.
Kingunge Ngambale Mwilu, akiweka shada la maua kwa niaba ya wazee.
Meya wa Ilala, Jerry Slaa,akiweka shada la maua.

RAIS WA ZANZIBAR DKT. SHEIN AZUNGUMZA NA WAFANYAKAZI WA OFISI YA MAKAMU WA KWANZA WA RAIS


 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi DK.Ali Mohamed Shein,(wa pili kulia) akizungumza na Uongozi wa Ofisi ya Makamo wa Kwanza wa Rais,katika kikao cha kujadili utekelezaji wa Mpango kazi wa Wizara hiyo,wa mwaka wa fedha 2013-2014 na robo ya kwanza ya mwaka wa fedha 2013-2014,katika Ukumbi wa Mikutano Ikulu Mjini Zanzibar,(kulia) Makamo wa Kwanza wa Rais Maalim Seif Sharif Hamad,(kulia) Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamo wa Kwanza  wa Rais Fatma Abdulhabib Fereji,(kusho) na Katibu Mkuu  Kiongozi DSk.Abdulhamid Yahaya Mzee.
Baadhi ya Viongozi mbali mbali wa Ofisi ya Makamo wa Kwanza wa Rais,wakiwa katika cha  kujadili utekelezaji wa Mpango kazi wa Wizara hiyo,wa mwaka wa fedha 2013-2014 na robo ya kwanza ya mwaka wa fedha 2013-2014,chini ya Mwenyekiti wake Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi DK.Ali Mohamed Shein,(hayupo pichani) katika Ukumbi wa Mikutano Ikulu Mjini Zanzibar.

PIKI PIKI YA MABONDIA NASSIBU RAMADHANI NA MOHAMED MATUMLA YAONESHWA

Meneja Masoko wa kampuni ya haojue,Wawa Laida kulia akiwaonesha pikipiki itakayogombaniwa Dar es salaam jana na mabondia Nassibu Ramadhani kushoto na Mohamed Matumla siku ya Desemba 25 katika ukumbi wa friends corner wengine wa pili kushoto ni Rashidi Matumla,Christopher Mzazi na mlatibu wa mpambano uho Kaike Siraju Picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com
Mratibu wa mpambano wa ndondi Kaike Siraju akiojiwa akiwa juu ya pikipiki itakayogombaniwa na mabondia Mohamed Matumla na Nassibu Ramadhani siku ya Desemba 25 Picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com
Meneja Masoko wa kampuni ya haojue,Wawa Laida kulia akiwaonesha pikipiki itakayogombaniwa Dar es salaam jana  na mabondia Nassibu Ramadhani kushoto na Mohamed Matumla siku ya Desemba 25  wengine wa pili kushoto ni Rashidi Matumla,Christopher Mzazi na mlatibu wa mpambano uho Kaike Siraju Picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com

Meneja Masoko wa kampuni ya haojue,Wawa Laida kulia akiwaonesha pikipiki itakayogombaniwa Dar es salaam jana  na mabondia Nassibu Ramadhani kushoto na Mohamed Matumla siku ya Desemba 25  wengine wa pili kushoto ni Rashidi Matumla,Christopher Mzazi na mlatibu wa mpambano uho Kaike Siraju Picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com

MABONDIA JAPHET KASEBA, ALIBABA KUZIPIGA DESEMBA 21 FRIENDS CORNER HOTEL DAR


Mabondia Japhet Kaseba wa jijini Dar es Salaam, na Alibaba Ramadhan wa jijini Arusha, wanategemea kupanda ulingoni siku ya jumamosi ya tarehe 21 Decemba, mwaka huu katika ukumbi wa friends corner hotel,kuzichapa katika pambano la kirafiki lisilo la ubingwa..
Pambano hilo liloandaliwa na Promota Ibrahim Kamwe chini ya  BigRight Promotion kwa usimamizi wa PST, pia litakuwa na mapambano  mengine tisa ya utangulizi ambayo yatawakutanisha mabondia kama Karage Suba na Fadhil Awadh, watakaozichapa kuwania ubingwa wa Mkoa katika uzito wa wealter Kg66 pambano la raundi kumi.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, leo Mratibu wa pambano hilo Ibrahim Kamwe, alisema kuwa  zaidi ya hayo mapambano ya ubingwapia mahasimu wawili wa uzito wa juu Lusekelo Daudi atazipiga na  Mbaruku Kheri (ndota) ikiwa ni marudio ya mchezo wao wa kusisimua uliokosa mshindi. 

Mabondia wengine watakaopanda ulingoni ni pamoja na Bondia Adam Yahaya (Baby Edo) atazipiga na Harman Richard, mkongwe Enerst Bujiku (Tyson) atacheza na Shah Kassim,  kukumbushia Enzi za akina Stanley Mabesi , Jocky Hamis mkongwe wa zamani atazipiga na bondia sawa na mwanae  mbena Rajabu.

Wengine ni Issa Omar  atazipiga na Haji Juma wa Tanga, Moro Best atapigana na Shafii Ramadhan, huku Shaban Bodykitongoji akizipiga na Mwinyi Mzengera. 

Mabondia wote wameshasaini mikataba ya makubaliano ya mchezo huo na wameshaingia kambini kujiandaa na mechi zao hizo ambazo zina upinzani wa hali ya juu.

kinachoendelea kwa sasa ni kumalizia mchakato wa ulinzi kutoka Kampuni ya Kiwango Security na jeshi la polisi.

JOSE CHAMELEONE ASAINI KUPIGA SHOW MOJA DEC 24 MKESHA WA CHRISTMAS JIJINI MWANZA


Mwanamuziki kutoka nchini Uganda Dr. Jose Chameleone akisaini mkataba wa wa kupiga show jijini Mwanza itakayofanyika mnamo tarehe 24/12/2013 mkesha wa kuikaribisha sikukuu ya Christmas kuanzia saa 12 jioni hadi majogoo, tukio linalotazamiwa kufanyika katika ufukwe wa Charcoal Ribs Mwanza.

Picha zaidi za Mwanamuziki mkali Afrika akisaini mkataba baina yake na viongozi waandaaji wa Show hiyo. Makubaliano haya ya kuweka mkataba yamefanyika jumatatu ya wiki hii tarehe 25/11/2013 jijini Kampalanchini Uganda.
Mwanamuziki Dr. Jose Chameleone (katikati) akiwa na Mapromota wa show itakayofanyika jijini Mwanza Dennis Mshema (Kushoto) na Mr. Ben Mwangi (kulia) mara baada ya utiaji wa saini wa kupiga show moja kali tena takatifu itakayofanyika mkesha wa kuikaribisha sikukuu ya Christmas katika ufukwe wa Charcoal Ribs jijini Mwanza.
 Kwa mujibu wa moja wa Mapromota hao Mr. Ben amesema kuwa ile kiu ya mashabiki wa muziki wa ukweli toka kwa Mwanamuziki Jose Chameleone sasa inakwenda kupata dawa yake, kwani maandalizi mazuri yameanza kufanyika kuhakikisha kila kilichobora kina tukia kwenye jukwaa la burudani siku hiyo ya mkesha wa Christmas.

"Tutafunga sound mpya ya mtikisiko, tutajenga jukwaa kubwa bora tena la kisasa, tutafunga taa za kisasa pamoja na huduma nzuri kwa wateja watakaofika ufukwe wa Charcoal Ribs Mwanza, nia na madhumuni kuufanya usiku huo kuwa mkubwa, mzuri wenye mengi maajabu katika burudani" Alisema Ben.

 Ameongeza kuwa bado milango iko wazi kwa makampuni mbalimbali na sekta binafsi kushiriki katika suala zima la udhamini. Kwa maelezo zaidi piga simu namba 0752813212.

Mbali na kuwa na masongi makali kama Bei kali, Kamila na kadhalika ambayo hadi sasa utamu wake uko pale pale Jose Chameleone kwa sasa anatikisa ulimwengu wa burudani ya muziki na ngoma zake kali kama Badilisha, Sumula, Valu valu, Tubonge na nyingine kibao...

Wednesday, November 27, 2013

SELCOM,VODA COM NA OIL COM WAUNGANA KURAHISISHA UNUNUZI WA MAFUTA KWA NJIA YA MPESA



Meneja wa huduma za Selcom,Bi,Everline Simpilu kushoto akitoa lisiti kwa mteja  wa mafuta wa kituo cha Oil Com Bw,Peter Ibrahimu wakati wa uzinduzi wa ununuaji wa mafuta kwa njia ya mtandao wengine wa pili kushoto ni Mkurugenzi wa Oil Com Bw,Mohamed Said Nahdi Ofisa wa Selcom Tumaini Mgori na Meneja husiano wa nje wa kampuni ya Vodacom Salumu Mwalimu huduma za kununua mafuta kwa njia ya mtandao zitakuwa zikitolewa na kampuni ya vodacom kupitia Mpesa ambapo uzinduzi huo ulifanyika Dar es salaam jana Kampuni ya Selcom ndio wawezeshaji na mashine zao  za POS ndio zitakazokuwa zikitumika picha na Mpiga picha  wetu

Meneja wa huduma za Selcom,Bi,Everline Simpilu kushoto akimpatia lisiti kwa mteja  wa mafuta wa kituo cha Oilcom Bw,Peter Ibrahimu wakati wa uzinduzi wa ununuaji wa mafuta kwa njia ya mtandao wengine wa pili kushoto ni Mkurugenzi wa Oilcom Bw,Mohamed Said Nahdi Ofisa wa Selcom Tumaini Mgori na Meneja husiano wa nje wa kampuni ya Vodacom Salumu Mwalimu huduma za kununua mafuta kwa njia ya mtandao zitakuwa zikitolewa na kampuni ya voda com kupitia Mpesa na mashine pekee za Selcom POS  uzinduzi huo ulifanyika Dar es salaam jana picha na Mpiga picha  wetu

Meneja wa huduma za Selcom,Bi,Everline Simpilu kushoto  akimweleza mwendesha bajaji Bw,Peter Ibrahimu  jinsi Selcom wanavyotoa huduma ya kununua mafuta kwa njia ya mtandao kwa kushirikiana na ,Vodacom Mpesa katika huduma ya lipa bidhaa pamoja na Oil Com

Meneja wa huduma za Selcom,Bi,Everline Simpilu kushoto Group IT meneja  wa Oil Com, Abubakari Mwita,Mkurugenzi wa Oil Com Bw,Mohamed Said Nahdi, Meneja husiano wa nje wa kampuni ya Vodacom Salumu Mwalimu.Ofisa wa Selcom Tumaini Mgori wakipata maelezo jinsi mashine ya Selcom inavyofanya kazi ya kununua mafuta kwa njia ya mtandao wakiungana na Oilcom na Vodacom  kupitia huduma ya lipa bidhaa  wakati wa uzinduzi uliyofanyika Dar es salaam jana picha na Mpiga picha  wetu
Ofisa wa Selcom Tumaini Mgori akiongea na wahandishi wa habari wakati wa huzinduzi wa huduma hiyo

Tuesday, November 26, 2013

YASSIN ABDALLAH MWAIPAYA -USTAADH AMPONGEZA CHEKA KUKIMBIA MBIO ZA UHURU MARATHON RAIS -TPBO


                             YASSIN ABDALLAH MWAIPAYA -USTAADH
                                                                          RAIS -TPBO  
                  NDG WAANDISHI NA WADAU WA MICHEZO WOTE KWA UJUMLA WETU,

AWALI YA YOTE NAPENDA KUTUMIA FURSA HII KUMPONGEZA BONDIA BINGWA WA DUNIA WA WBF,FRANCIS CHEKA KWA KUKUBALIANA NA WAZO LANGU LA KUMUOMBA AJIUNGE NA KUWA MIONGONI MWA WATANZANIA WATAKOJITOKEZA TAREHE 08-12-2013 JIJINNI DAR-ES0SALAAM KUUNGANA NA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO YA TANZANIA MH, JAKAYA MRISHO KIKWETE KUKIMBIA MBIO ZA UHURU MARATHON ZENYE KUADHIMISHA UHURU WA TANGANYIKA.

KWA KWELI NILIKUWA NA MATEGEMEO MAKUBWA SANA KWAMBA FRANCIS CHEKA ANGENIKUBALIA WAZO LANGU HILO ,AKIWA KAMA NI MTANZANIA ANAYEIPENDA KWA DHATI NCHI YAKE KWANI AMESHAIPATIA SIFA KUBWA TANZANIA KWA KUTWAA TAJI LA UBINGWA WA NGUMI WA DUNIA  DHIDI YA MMAREKANI PHILL WILLIAM HAPO TAREHE 30-08-2013 .

NA NILISHAWISHIKA KUMSHAURI CHEKA AINGIE KWENYE MBIO HIZI BAADA YA KUVUTIWA NA TAARIFA ZA WAANDAAJI KWAMBA KATIKA MBIO HIZO YUMO BINGWA WA DUNIA WA MBIO HIZO KUTOKA KENYA, NIKAONA IKO HAJA KWA  MABINGWA WA TASNIA ZISIZOFANANA  WAKANOGESHA MBIO HIZI ZA UHURU MARATHON HAPO 08-12-2013 PALE LEADERS CLUB.

NINAONA WAZI KWAMBA SASA IPO HAJA HATA  KWA MAKAMPUNI MBALIMBALI YAKAMTUMIA FRNCIS CHEKA KATIKA SHUGHULI ZAO MBALIMBALI ZA KIJAMII NA HATA KUWATANGAZIA BIASHARA ZAO.

KWA KWELI HIZI NI MBIO AMBAZO ZINAPASWA KUUMGWA MKONO NA KILA MTANZANIA NA SIYO WANARIADHA PEKEE ,KWANI HAYATI BABA WA TAIFA HILI MWL JULIUS KAMBARAGE NYERERE ALIUPIGANIA UHURU WA NCHI HII KWA MASLAHI YA WATANZANIA WOTE, BILA KUJALI ITKADI ZA KIDINI, ZA KIMICHEZO ,NA HATA UKABILA.

NI JAMBO LA KUTIA MOYO KWAMBA WAMEJITOKEZA WATANZANIA WENYE NIA NJEMA KABISA YA KUUENZI UHURU WA TANGANYIKA KWA NJIA YA MICHEZO [KAMA HAWA WAANDAAJI WA UHURU MARATHON].

NI LAZIMA TUWAUNGE MKONO WAANDAAJI HAWA KWA HALI NA MALI ILI TUUENZI VYEMA UHURU WETU.

NINATUMIA FURSA HII KUWAOMBA MABONDIA WENGINE NA WADAU WA MCHEZO WA NGUMI  WAJIUNGE KWENYE MBIO HIZI KWA LENGO MOJA TU NALO NI KUUENZI UHURU WA NCHI YETU ,KWANI BILA KUWA NA UHURU KTK NCHI YOYOTE , WAZALENDO WA NCHI ILE HUWA HAWANA TOFAUTI NA WATUMWA,KWANI WANAKUWA HAWANA MAAMUZI YAO BINAFSI ,KWA KUWA KILA JAMBO HUAMULIWA  NA WATAWALA WAO BILA KUJALI JAMBO NI ZURI AU BAYA.

KWA KUWA WAANDAAJI WAMETUTANGAZIA KUPITIA VYOMBO MBALIMBALI VYA HABARI KWAMBA KUNA MATAIFA ZAIDI YA 21 YAMETHIBITISHA KUSHIRIKI KATIKA UHURU MARATHON ,PIA MHESHIMIWA RAIS,NA WABUNGE , WAMETHIBITISHA USHIRIKI WAO,SIONI KWA NINI WATANZANIA WA KAWAIDA TUSISHIRIKI KATIKA TUKIO HILI LA KIHISTORIA LA UHURU MARATHON.

PIA NINAYAOMBA MAKAMPUNI MBALIMBALI YAZIDHAMINI MBIO HIZI ZA UHURU MARATHON KILA MWAKA ,NA ISIWE MWAKA HUU PEKEE.

NINA IMANI KUBWA SANA KWAMBA WATANZANIA WENGI TUTASHIRIKI MBIO HIZI ZA UHURU MARATHON SIKU HIYO YA TAREHE 08-12-2013 PALE LEADERS CLUB.


              MUNGU IBARIKI TANZANIA NA WATU WAKE ,NA UDUMISHE UHURU NA AMANI NCHINI KWETU TANZANIA.


                                        IMELETTWA KWENU NAMI;-
                                       YASSIN ABDALLAH -USTAADH
                                       RAIS; TPBO-LTD
                                     +255 713-644974 752 335584

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AFUNGUA KONGAMANO LA NCHI WANACHAMA WA SHIRIKISHO LA VIWANDA VYA UTENGENEZAJI NGUO KWA NCHI WANACHAMA WA JUMUIYA YA MADOLA BARANI AFRIKA (CAPA)


 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akikata utepe kuzindua rasmi Jarida la Wanachama wa Shirikisho la Viwanda vya Utengenezaji nguo kwa nchi Wanachama wa Jumuiya ya Madola Barani Afrika (CAPA Journal), wakati wa ufunguzi wa Kongamano hilo lililoanza leo katika Ukumbi wa AICC jijini Arusha. Kushoto ni Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dkt. Shukuru Kawambwa na (kulia) ni Mwenyekiti wa Bodi ya CAPA,John Kondoro. 
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisoma hotuba yake ya ufunguzi wa Kongamano la Nchi Wanachama wa Shirikisho la Viwanda vya Utengenezaji Nguo kwa nchi Wanachama wa Jumuiya ya Madola Barani Afrika,lililoanza leo katika Ukumbi wa AICC jijini Arusha.
 Baadhi ya washiriki wa Kongamano hilo, wakiwa makini kumsikiliza Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, wakati alipokuwa akisoma hotuba ya ufunguzi.
 Baadhi ya washiriki wa Kongamano hilo, wakiwa makini kumsikiliza Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, wakati alipokuwa akisoma hotuba ya ufunguzi.
 Baadhi ya washiriki wa Kongamano hilo, wakiwa makini kumsikiliza Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, wakati alipokuwa akisoma hotuba ya ufunguzi.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akipokea zawadi ya Kinyago kutoka kwa Makamu wa Mwenyekiti wa CAPA wa Kanda ya Afrika Magharibi, Prof. Daniel Nyarko, baada ya kufungua rasmi Kongamano la Nchi Wanachama wa Shirikisho la Viwanda vya Utengenezaji Nguo kwa nchi Wanachama wa Jumuiya ya Madola Barani Afrika,lililoanza leo katika Ukumbi wa AICC jijini Arusha.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal (wa nne kushoto), Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dkt. Shukuru Kawambwa (wa pili kushoto), Mwenyekiti wa Bodi ya CAPA,John Kondoro (kushoto kwa Makamu) na baadhi ya viongozi wa CAPA, wakifurahia kwa pamoja baada ya kuzindua rasmi Jarida la Wanachama wa Shirikisho la Viwanda vya Utengenezaji nguo kwa nchi Wanachama wa Jumuiya ya Madola Barani Afrika (CAPA Journal), wakati wa ufunguzi wa Kongamano hilo lililoanza leo katika Ukumbi wa AICC jijini Arusha.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya washiriki wa Kongamano hilo. 
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya washiriki wa Kongamano hilo. 
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya washiriki wa Kongamano hilo. 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akifurahia burudani ya ngoma ya Kimasai, wakati akitoka kwenye Ukumbi wa AICC, baada ya kufungua rasmi Kongamano la Wanachama wa Shirikisho la Viwanda vya Utengenezaji nguo kwa nchi Wanachama wa Jumuiya ya Madola Barani Afrika (CAPA Journal)lililoanza leo katika jijini Arusha.
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...