Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Saturday, February 15, 2014

Ngassa azidi kung'ara Afrika apiga hat trick nyingine Comoro, Chuoni yang'oka Shirikisho Afrika yalala kwa Wazimbabwe



https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgs5ridVRJd__Uy-JxogsvGOhrSJKff2Ge0jAyos63qLr-SJ6nfltaez51GStW-jrTVlFyTFUOoF8z5xAP46_H9ASwRGnbOs-Sjh8bBDv15_hoSFp5EdnNQIgj_Rgjy5_7urUj8Dr0446H4/s640/blogger-image-1980253589.jpg
Ngassa alipoinyanyasa Komorozine jijini Dar na leo kaifanyia hivyo hivyo kwa kupiga hat trick

WINGA machachari wa kimataifa, Mrisho Ngassa ameendelea kuweka rekodi Afrika baada ya jioni ya leo nchini Comoro kufunga hat trick nyingine na kuondoka na mpira wakati Yanga ikiilaza Komorozine de Domoni kwa mabao 5-2.
Ngassa alifunga mabao matatu katiuka mchezo wa kwanza wakati Yanga ikishinda mabao 7-0 na kuondoka na mpira uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na kurudia kitendo hicho leo inamfanya kufikisha jumla ya mabao 6 na kuongoza kwenye orodha ya wafungaji wa michuano hiyo ya Ligi ya Mabingwa Afrika.
Mabao mengine ya Yanga katika mchezo huo wa marudiano yaliwekwa kimiani na Simon Msuvah na Hamis Kiiza 'Diego'.
Kwa ushindi huo Yanga imefuzu raundi ya kwanza kwa jumla ya mabao 12-2 na kupata nafasi ya kuvaana na mabingwa watetezi wa michuano hiyo, Al Ahly ya Misri katika mechi mbili kazi inayoonekana ngumu kwa mabingwa hao watetezi wa Ligi Kuu Tanzania Bara.
Nao wawakilishi wa Tanzania Zanzibar katika michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika Chuoni, imehitimisha safari yake katika michuano hiyo baada ya kulazwa mabao 2-1 na How Mine ya Zimbabwe katika mchezo uliochezwa uwanja wa Amaan Zanzibar.
Chuoni walitangulia kupata bao kabla ya wageni kurejesha na kuongeza la ushindi na kufanya isonge mbele kwa jumla ya mabao 6-1 baada ya mechi ya awali Wazimbabwe hao kushinda nyumbani mabao 4-0.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...