Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Sunday, February 16, 2014

TAMWA Yawapongeza Wanahabari Uandishi Habari za Ukatili wa Kijinsia


Mkurugenzi Mtendaji wa Chama cha Wanahabari Wanawake (TAMWA), Valerie Nsoka  akizungumza na wahariri na waandishi wa habari  (hawapo pichani)  leo Makao Makuu ya Ofisi hizo, Sinza Jijini Dar es Salaam. Mkurugenzi Mtendaji wa Chama cha Wanahabari Wanawake (TAMWA), Valerie Nsoka akizungumza na wahariri na waandishi wa habari (hawapo pichani) leo Makao Makuu ya Ofisi hizo, Sinza Jijini Dar es SalaamMkurugenzi Mtendaji wa Chama cha Wanahabari Wanawake (TAMWA), Valerie Nsoka akizungumza na wahariri na waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali vya habari (hawapo pichani) jijini Dar es Salaam. Mkurugenzi Mtendaji wa Chama cha Wanahabari Wanawake (TAMWA), Valerie Nsoka akizungumza na wahariri na waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali vya habari (hawapo pichani) jijini Dar es Salaam.Sehemu ya wahariri na waandishi wa habari waandamizi kutoka vyombo mbalimbali vya habari nchini. Sehemu ya wahariri na waandishi wa habari waandamizi kutoka vyombo mbalimbali vya habari nchini wakiwa katika mkutano huoSehemu ya wahariri na waandishi wa habari waandamizi kutoka vyombo mbalimbali vya habari nchini. Sehemu ya wahariri na waandishi wa habari waandamizi kutoka vyombo mbalimbali vya habari nchini wakifuatilia mada katika mkutano huoMmoja wa wahariri kutoka magazeti ya Uhuru na Mzalendo, Lilian Timbuka (wa kwanza kushoto) akichangia mada katika mkutano huo. Mmoja wa wahariri kutoka magazeti ya Uhuru na Mzalendo, Lilian Timbuka (wa kwanza kushoto) akichangia mada katika mkutano huo.Sehemu ya wahariri na waandishi wa habari waandamizi kutoka vyombo mbalimbali vya habari nchini. Sehemu ya wahariri na waandishi wa habari waandamizi kutoka vyombo mbalimbali vya habari nchini.

MKURUGENZI Mtendaji wa Chama cha Wanahabari Wanawake (TAMWA), Valerie Nsoka amevipongeza vyombo vya habari kwa kutoa ushirikiano wa uandishi wa habari za ukatili wa kijinsia ambao umeonesha mafanikio kwa sasa ukilinganisha na mwamko uliokuwepo miaka ya nyuma.

Bi. Nsoka ametoa kauli hiyo leo jijini Dar es Salaam alipokuwa akiwasilisha taarifa ya matokeo ya utafiti wa mradi wa GEWE II (Mpango wa kutokomeza ukatili na unyanyasaji wa kijinsia dhidi ya wanawake na watoto) kwa wahariri na waandishi wa habari waandamizi kutoka vyombo mbalimbali vya habari nchini.

Alisema kwa kipindi cha kuanzia Oktoba 2012 hadi Septemba 2013, jumla ya habari 499 ziliandikwa kwenye magazeti mbalimbali kupitia mradi wa GEWE, huku habari 216 zikiandikwa kwenye miradi mingine ya taasisi hiyo hivyo kufanya idadi ya habari zote kufikia 715 kwa mwaka.

Alisema ongezeko hilo limeleta mafanikio kadhaa kwa jamii hivyo kuwaomba waandishi wa habari waongeze juhudi za uandishi wa habari za ukatili wa kijinsia ili kukomesha vitendo hivyo vinavyo endelea kuiathiri jamii.

"...Hali inaonesha uchapishaji wa habari uliongezeka zaidi kwa vitendo vya ukatili, ukilinganisha na kipindi cha mwaka 2012 ambapo uchapishaji wa habari katika magazeti ulikuwa na Idadi ya 350 kwa miradi yote ya TAMWA," alisema Mkurugenzi huyo.

Alisema ongezeko hilo la uandishi wa habari za ukatili wa kijinsia limeleta mafanikio kwa kiasi fulani, kwani kwa sasa jamii imepata uelewa kuhusu masuala ya ukatili wa kijinsia na waliokuwa wakinyanyasika sasa wamejitokeza kuomba msaada zaidi.

"...TAMWA imekua ikipokea simu kutoka sehemu mbalimbali za Tanzania watu wakiomba msaada wa kutatuliwa matatizo yao. Kituo ha usuluhishi cha TAMWA kimekua kikipokea watu wakisema wamepata habari baada ya kusoma au kuona machapisho au tangazo kupitia luninga au kusikiliza redio...," alisema Bi. Nsoka.

Aidha alisema waandishi wa habari wa Dar es salaam na mikoa mingi sasa wameweza kuandika na kutangaza habari mbalimbali za ukatili wa kijinsia kwa ufasaha.

Akizungumzia matokeo ya utafiti wa kihabari uliofanywa na TAMWA kwa kushirikiana na waandishi wa habari, alisema utafiti ulibaini kuwa asiliamia 17 ya wananchi hawana uelewa wa sheria za ukatili wa kijinsia, huku Mkoa wa Lindi kupitia Wilaya ya Lindi Vijijini ikiongoza kwa kupata asilimia 12.

Alisema utafiti huo uliowahoji jumla ya watu 2,300 pia ulibaini kuwa asilimia 47 za kesi huripotiwa katika Serikali za vijiji na asilimia 25 huripotiwa katika vituo vya polisi. Utafiti ulinesha kuwa wananchi hawana majukwaa ya kukaa pamoja na kujadili changamoto zao ambapo ni asilimia 13.5 ndiyo wanachama wa asasi za kijamii.

TAMWA kwa kushirikiana na vyombo mbalimbali vya habari kiliwatuma waandishi wa habari kwenda katika Wilaya 10 za mradi na kufanya utafiti ambao matokeo yake yalitolewa mwezi Julai 2013. Wilaya 10 za Tanzania Bara na Visiwani, ni pamoja na Kinondoni, Ilala, Kisarawe, Mvomero, Ruangwa, Lindi Vijijini, Newala, Wete, Unguja Mjini Magharibi na Unguja Kusini.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...