Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Thursday, June 19, 2014

HUDUMA YA TRENI YA ABIRIA YA BARA KUANZA TENA JUMANNE JUNI 24, 2014


 Uongozi wa Kampuni ya Reli Tanzania – TRL unafuraha kuwataarifu  abiria wote na wananchi kwa jumla  kuwa kutokana na kukamilika ukarabati wa daraja eneo la bonde la mto Ruvu mkoani Pwani huduma ya treni ya abiria itaanza upya hapo siku ya Jumanne Juni 24, 2014 kutoka Stesheni ya Dar es Salaam saa 11 jioni. Wananchi wanotaka kusafiri wafike stesheni zilizo
karibu yao kwa ajili ya kukata tiketi kuanzia 
Juni 19, 2014.

Halikadhalika muda wa kuondoka treni kwa siku za Jumanne na Ijumaa kutoka Stesheni ya Dar kwenda Kigoma na Mwanza utakuwa saa 11 jioni na zile za kutoka Kigoma na Mwanza kuja Dar  katika siku za Alhamis na
Jumapili ni saa 11 jioni  kutokea Kigoma na saa 12 magharibi kutokea Mwanza.
                                                                                         
 Tafadhali atakayesoma taarifa hii  amuarifu na mwenzake. Uongozi wa TRL unawapongeza wananchi kwa ujumula kwa ushirikiano na uvumilivu waliouonesha wakati wakisubiri kukamilika kwa kazi ukarabati wa njia ya reli.

Imetolewa na Ofisi ya Uhusiano ya
TRL kwa Niaba ya 
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji ,
Mhandisi  Elias Mshana
Dar es Salaam,
Juni 18, 2014.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...