Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Sunday, September 28, 2014

MASHINDANO YA SKAUTI NGAZI YA TAIFA YAFUNGWA RASMI MKOANI MOROGORO


 Kamishina Mkuu Msaidizi Programu ya Vijana wa Chama cha Skauti Tanzania (TSA), Mary Anyitike (kushoto), akimvisha  Nishani ya Skauta, Safi Shabani kiongozi wa Skauti kutoka  Shule ya Sekondari Lugoba iliyopo Bagamoyo mkoa wa Pwani wakati wa hafla ya kufunga mashindano hayo jana.
 Kamishina Mkuu Msaidizi wa Utawara Bora wa Chama cha Skauti Tanzania (TSA), Mwalimu mstaafu John Lusunike (kushoto), akikagua skauti kabla ya kuanza mashindano Septemba 23,2014. 
 Vijana wa Skauti wa Mkoa wa Dar es Salaam wakiwa tayari kwa ukaguzi.
 Vijana wa Skauti wa Kikosi cha Simba kutoka Mkoa wa Morogoro ambao walikuwa washindi wa Mashindano ya Skauti katika nchi za Afrika Mashariki yaliyofanyika nchini Burundi mwaka 2013 wakiwa tayari kwa ukaguzi huo kabla ya mashindano hayo yenye lengo la kuwapata washiriki katika mashindano ya Afrika Mashariki yatakayofanyika nchini Rwanda Desemba 2014.
 Vijana wa Skauti wakijifunza Kilimo Hai jinsi ya kuandaa shamba mfuko bila kutumia mbolea zisiso na kemikali.
 Vijana wa skauti wakiwa katika maandalizi ya kupangiwa kazi.
 Vijana wa skauti wakionesha namna ya kutoa huduma ya kwanza kwa mtu aliyepoteza fahamu.
 Hapa vijana wa skauti wakipika chai wakiwa juu ya mti.
 Vijana wa skauti wakijadili maswali ya kazi walizopewa.
 Hapa wakiwa wamepumzika kwenye vitanda vya miti.
 Vijana hao wakisubiri kupatiwa maelekezo na viongozi wao.

 Kamishina wa Skauti Mkoa wa Morogoro, Francis Gasper Francis kwa niaba ya Kamisha Mkuu wa TSA, akimuapisha Kamishina wa Wilaya ya Kilosa ndugu Miraji.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...